Je, unaweza kulala ndani ya dakika mbili?

Watu wengine huwa na wakati mgumu kulala, wakati wengine hawawezi kulala kabisa. Mamilioni ya watu ulimwenguni kote wanakabiliwa na tatizo hili.

Kila mtu anajitahidi kulala haraka. Baadhi ya tafiti zimeonyesha kuwa kati ya asilimia tano hadi hamsini ya watu wanakabiliwa na tatizo la kukosa usingizi.


Watu wengine wanaendelea kugeuka kutoka upande mmoja hadi mwingine usiku kucha. Lakini hawawezi kulala. Kisha tafiti zinafanywa ili kuona ikiwa kuna njia zozote za kuwasaidia kulala. Baadhi ya mbinu zimependekezwa. Lakini kwa sasa, Mbinu ya Kulala Kijeshi inajadiliwa kwa kiwango kikubwa.

Savvy Media

Njia hii imeenea kwenye majukwaa mengi ya mitandao ya kijamii, ikiwemo TikTok, na video zake zimekuwa zikipata mamilioni ya maoni.

Inadaiwa kuwa ukitumia mbinu hii, utalala ndani ya dakika mbili.

Lakini wataalam, wakizungumza na Idhaa ya Dunia ya BBC, wameelezea wasiwasi wao kwamba hii inaweza kuharibu usingizi kwa sababu inaleta matarajio yasiyowezekana.

Wataalamu pia waliambia Idhaa ya Dunia ya BBC kuhusu vidokezo halisi vya kulala kutoka kwa wanajeshi ambavyo watu wa kawaida wanaweza kujaribu.

Post navigation

Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Ikiwa unapenda chapisho hili unaweza kupenda haya

error: Content is protected !!