Mimi ni kipara, na hali hii imenitatiza kwa muda mrefu..
Hata hivyo, kilichonisumbua zaidi si upara wenyewe, bali kutoridhika kwangu na hali hiyo.
Mtazamo mmoja tu wa ukurasa wangu wa Instagram unaonyesha wazi kwamba mimi si mwanaume pekee ninayejali na kuathirika kihisia kuhusu nywele zake.
Savvy Media
Kila ninapofungua Instagram, nakumbana na wingi wa video na machapisho yanayotangaza upandikizaji wa nywele, vidonge vya kuchochea ukuaji wa nywele, dawa za kuongeza wingi, poda za kuficha sehemu zilizoathirika na upara, pamoja na nywele bandia zinazouzwa kwa majina mapya.
Bidhaa na huduma hizi zote zinaahidi kurejesha “kujiamini kulikopotea” na kuhakikisha kwamba kupoteza nywele “hakutakuwa kikwazo katika maisha.”
Swali linalojitokeza ni kama wingi wa chaguo hizi unaashiria mabadiliko ya mtazamo kuhusu upara. Je, jambo ambalo hapo awali lilichukuliwa kama hali ya kukubalika sasa limegeuka kuwa tatizo linaloweza kurekebishwa ingawa kwa gharama kubwa?




Leave a Comment