Juventus inawataka nyota hawa wa Liverpool na Man U

Nottingham Forest wametoa ofa ya pauni milioni 35 kumsajili mshambuliaji wa Crystal Palace, Jean-Philippe Mateta, lakini Palace (Eagles) wanataka kifurushi cha pauni milioni 40 na watamruhusu Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 28 kuondoka ikiwa bei hiyo itafikiwa. (Athletic)

Juventus pia wanavutiwa na winga wa Liverpool, Mtaliano, Federico Chiesa, 28, na mshambuliaji wa Uholanzi Joshua Zirkzee, 24, ambaye yuko Manchester United . (Gazzetta dello Sport)


Mshambuliaji wa Everton na Guinea-Bissau Beto, 27, ni mojawapo ya chaguo la Juventus wanapotafuta kumsajili mshambuliaji wakati wa dirisha la uhamisho la majira ya baridi. (Gazzetta dello Sport)

Savvy Media

Mshambuliaji wa Ufaransa Randal Kolo Muani, 27, yuko Tottenham kwa msimu mzima akitokea Paris St-Germain na ni chaguo jingine ambalo Juventus wanalitazama (Fabrizio Romano)

Post navigation

Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Ikiwa unapenda chapisho hili unaweza kupenda haya

error: Content is protected !!