AFCON 2025: Nguvu ya makocha wa Afrika yaonekana

Nani kati ya makocha hawa wa Afrika, Pape Thiaw (Senegal), Hossam Hassan (Misri), Walid Regragui (Morocco) au Eric Chelle (Nigeria) atatwaa ushindi Kombe la Mataifa ya Afrika 2025?

Baada ya kumalizika kwa robo fainali, kulikuwa na jambo moja la hakika; kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) litabaki mikononi mwa kocha kutoka bara hili.


Kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa AFCON mwaka 1957, timu nne zilizofika nusu fainali, Senegal, Misri, Nigeria na Morocco, zote zinaongozwa na makocha raia wa Afrika.

Savvy Media

Mmoja kati ya Pape Thiaw, Éric Chelle, Hossam Hassan na Walid Regragui, atakuwa bingwa wa Afrika tarehe Januari 18, 2026.

Tangu 2019, Kombe la Mataifa ya Afrika limekuwa na mabadiliko kwa makocha Waafrika. Djamel Belmadi aliiongoza Algeria kushinda mwaka 2019, Aliou Cissé aliipa Senegal taji lake la kwanza mwaka 2021, na Emerse Faé aliiongoza Ivory Coast kushinda mwaka 2023.

Zaidi ya hayo, AFCON ya 2025 inaashiria mabadiliko makubwa katika soka na uthibitisho kuwa soka la Afrika linazidi kuwa huru, na makocha wake sasa wana uwezo wa kushindana, si tu barani bali pia duniani kote

Katika hatua ya makundi: kati ya timu 24 zilizoshiriki, 15 zilisimamiwa na makocha wa Kiafrika. Raundi ya 16: Makocha 11 ni kutoka Afrika kati ya timu 16 zilizofuzu.

Robo fainali: Makocha 6 ni kutoka Afrika kati ya 8, ni Mbelgiji Tom Saintfiet (Mali) na Mswisi Vladimir Petkovic (Algeria) pekee ndio ambao hawakuwa wazawa.

Post navigation

Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Ikiwa unapenda chapisho hili unaweza kupenda haya

error: Content is protected !!