Katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika iliyojaa utata, Brahim Diaz wa Morocco alikosa penalti, baada ya dakika 17 za kusimama kwa mpira kuelekea kipenga cha mwisho.
Mshambuliaji huyo wa Real Madrid alipunguza mwendo alipokaribia mpira na kuupiga katikati ya goli lakini kipa Edouard Mendy wa Senegal hakuruka pembeni, aliudaka mpira na mchezo ukaendelea hadi muda wa ziada na Senegal ikaibuka na ushindi.
Ilikuwa siku mbaya kwa Diaz, aliyeonekana na huzuni alipokabidhiwa kiatu cha dhahabu kama mfungaji bora wa mashindano hayo na rais wa Fifa, Gianni Infantino mwishoni mwa mchezo.
Savvy Radio
Sio mara ya kwanza kwa mchezaji kukosa goli kwa kupiga penalti katikati ya goli, penalti inayoitwa Panenka.

Penalti kama hiyo ya Enzo le Fee wa Sunderland ilinaswa na Caoimhin Kelleher katika mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Brentford mapema Januari.
Je, kupiga penalti katikati ya goli ndio chaguo baya zaidi kwa mkwaju wa penalti?









Leave a Comment